NJIA ADIMU ZA KUONGEZA WATEMBELEAJI KWENYE BLOG YAKO

27, 2013   New Bies, Trainings   4 Comments
blog traffic

Kama tayari umeshafungua Blog yako, basi hongera kwa hilo kwani hiyo ni hatua kubwa ambayo kila Blogger aliyefanikiwa amepitia. Sasa kinachofuata ni nini cha kufanya ili kuhakikisha watu wanaokuja kutembelea Blog yako hawakauki na wanaongezeka kila leo. Lazima tuwe na dhamira ya kufika mbali na kwamba tumeamua ku blog ili tupate kipato na si vinginevyo, japokuwa tunaweza kufungua blog kama sehemu ya Kujifurahisha lakini furaha hiyo italeta tija kama una kipato kinapatika ndani ya kujifurahisha huko.
Zifuatazo ni Miongoni mwa mbinu Unaweza zitumia Blogger ili kujihakikishia watembeleaji wa kudumu na wapya kuongezeka kila leo:-
1.Kuandika Mada/Topic nzuri zenye kuvuta hisia.
Hii ni muhimu sana kwani baada ya kutambua wasomaji/wafutiliaji wako basi yafaa kutambua ni mada gani zinawagusa zaidi na zitawafanya warudi kila leo.


2.Kuchangia katika blog nyingine za kufanana na yako
Pia uwe na tabia ya kutoa comment au kutoa mada katika blog nyingine zenye muingiliano na yako huku ukiacha link ya mada zako katika blog hizo.
3.Kutumia vizuri SEO Tools ili kupatikana kirahisi mtandaoni
Zipo SEO Tools nyingi za bure ambazo husaidia blog yako kupatikana kirahisi mtandaoni kupitia keywords katika search engines mfano Google, miongoni mwa hizo ni Attracta.
4.Kujitanua ki network kupitia Mitandao ya kijamii mfano Facebook.


Kupitia mitandao hii unaweza kupata wafuatiliaji wa kutosha kwani wengi tayari huwa ni marafiki au jamaa zako, pia huwa na element ya kutaka kuona ni jinsi gani mwenzao unafanya.
5.Uwe na ratiba nzuri yak u post, usikae kimya muda mrefu.


Ikiwa umefungua Entertainment Blog, News Blog au Gossip Blog basi zisipite siku mbili bila ku post vitu vipya katika blog yako ili watu wawe na imani ya kupata kile wanachokitarajia katika blog hiyo, lakini ikiwa ni education au informative blog basi hata siku nne si mbaya.
6.Topic zako zisiwe nje ya Muonekano wa blog yako (Niche)
Kama ni taarifa basi ziwe taarifa za kweli, si za kutunga na ziwe zina uhusiano na Dira ya Blog yako, usitoke nje ya mada na uwe na Dira yenye tija.
7.Usiweke “MAVITU” Mengi Katika Blog yako kwani Huweka uzito wa Ku load.
Si kila Plugin ni nzuri kwa blog yako, nyingine hufanya pages zako ku load taratibu mno, hii huwakera wanaokuja kutembelea blog yako.

Kwa haya machache ukifuatilia nnaimani utafika mbali katika blogging.
Tafadhali Toa Maoni yako.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment